Friday 16 September 2011

hivi ndivyo soko la mwanjelwa mbeya lilivyoteketea kwa moto leo

Soko la mwanjelwa linavyoteketea kwa moto eneo la sido jijini mbeya,chanzo cha moto huo mpaka sasa hakijajulikana
Moto mkubwa ukiendelea kuwaka
Baadhi ya  mabanda sokoni hapo tayari yameteketea kabisa na moto

Kama kawaida kikosi cha maigizo cha zimamoto mbeya kimeendeleza libeneke la maigizo yake ya kwenda kwenye tukio na gari bovu ambalo hata maji ya kuzimia moto huo halina.na hapa wanaonekana askari wa kikosi hicho wakibishana huku moto ukiendelea 
Kufa kufaana....... kibaka tayari ameshaiba na huyooo anatimka zake.
Dada nae hayuko nyuma katika la kujisevia bidhaa sokoni hapo, keshachukua kapeti na kutokomea nalo.
Umati wa watu ukiwa unaangalia soko linavyoteketea
Mama huyu akilia kwa uchungu akiangalia duka lake likiteketea kwa moto

Hii ni hatari.

Moto ulianza pale majira ya asubuhi  Saa 3:50, lakini mpaka kufikia saa 5:15 Zimamoto walikuwa bado hawajafika na walipofika wakaaza kuzima moto ulikoanzia badala ya kule uelekeapo ili kunusuru mali nyingine zisiteketee.
 Na baadhi ya wafanyabiashara wamefanikiwa kuokoa bidhaa zao lakn waliowengi wamepata hasarA
Soko la Sido Mwanjelwa Jijini Mbeya ambapo chanzo cha Moto hiyo ni hitilafu ya umeme.
 Mto unaendelea kuteketeza bidhaa
Moto mkubwa ukiendelea kuwaka















 Masalia ya Bati zilizoteketezwa na Moto katika Soko la Sido.
 Gari la zima ambapo wananchi wakikinga maji kwa lengo la kusaidia kuzima maji vibanda vyao.
 Askari wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT akiwa amemkamata mualifu ambaye alikuwa akijaribu kuiba bidhaa sokoni Hapo.
 Askari wa JKT wakimuadhibu mualifu au Kibaka
 Askari wa JKT na Polisi wakiwa wameweka chini ya Ulinzi kibaka.
Wezi na vibaka wafurahia tukio wakiwemo akina mama hili kwani imekuwa fursa kwao kutokana na kujinufaisha kwa kuiba ikumbukwe katika ajali iliyopita ya Soko la Mwanjelwa watu weki walipata mitaji kutokana na kuiba mali.

Moto ukiendelea kuchoma vibanda na makontena ya Biashara sokoni hapo.
















Picha kwa Hisani ya Mbeya Yetu Blog na Latest News Tz Blog.

No comments:

Post a Comment