Sunday 23 October 2011

UN FAMILY DAY YAFANA KATIKA VIWANJA VYA LEADER'S CLUB JIJINI DAR ES SALAAM JUMAMOSI

 Kandanda
 Wazazi wakionekana kufurahi na watoto wao katika mkusanyiko huo uliokutanisha Familia za Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Kucheza pamoja, kula pamoja, kunywa pamoja na kushiriki michezo mbalimbali.
 Familia zikiwa pamoja.
 Mgeni rasmi Mkuu wa Itifaki Balozi A. Itatiro akizungumza machache wakati wa UN Family Day na kusema kwamba siku hiyo haikuwa ya kusoma risala bali ni siku ya kufurahi pamoja....Happy Birthday UN..!!!
 JAMANI NYIE VIPI JIPANGENI BASI  TUANZE JUA KALI: Ililfika zamu ya Wakubwa kupimana nguvu katika mchezo wa kuvuta kamba baina ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa.

 Timu ya Umoja wa Mataifa Vuta nikuvute....!!!
 Ushindi ukaibukia kwa UN huku Wizara ya Mambo ya Nje ikala kwao.
 Timu ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
 Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Bw. Alberic Kacou akionekana kufurahishwa na ushindi wa Vijana wake.
 MC akiongoza Wafanyakazi wenzake katika kucheza KWAITO.
 Vikombe kwa ajili ya washindi wa mechi kati ya UN na Wizara ya Mambo ya Nje.

Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Bw. Alberic Kacou akiteta jambo na mgeni rasmi Mkuu wa Itifika  Balozi A. Itatiro  huku MC akiendelea na utaratibu wakati wa kutoa Vikombe kwa washindi.

Kapteni wa timu ya Mpira wa Miguu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Kikombe cha Ushindi.
 Pichani Juu Kapteni wa timu ya Mpira wa Miguu ya Umoja wa Mataifa akipokea kikombe cha ushindi wakati wa mchezo wa kuvuta kamba kwa niaba ya wafanyakazi wenzake kutoka kwa mgeni rasmi Mkuu wa Itifika  Balozi A. Itatiro. Chini  UN Oyeee....
  Kapteni wa timu ya Mpira wa Miguu ya Umoja wa Mataifa 
 Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika picha ya pamoja na kikombe chao.
 Menyu
 Ongeza..Ongeza.....
 Chilli sosi iko wapi jamani....
 Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Alberic Kacou (wa pili kulia) akiwa na Vijana wake wa kazi.
 Kwaito...
 Kwaito likiendelea
Hoyce Temu katika picha ya pamoja na binti ambaye angependa kuwa kama yeye hapo baadaye.

No comments:

Post a Comment